1 Nya. 2:2-9 Swahili Union Version (SUV)

2. na Dani, na Yusufu, na Benyamini, na Naftali, na Gadi, na Asheri.

3. Wana wa Yuda; Eri, na Onani, na Shela; ambao hao watatu alizaliwa na binti Shua, Mkanaani. Naye Eri, mzaliwa wa kwanza wa Yuda, alikuwa mbaya machoni pa BWANA; naye akamwua.

4. Na Tamari, mkwewe, akamzalia Peresi, na Zera. Wana wote wa Yuda ni watano.

5. Wana wa Peresi; Hesroni, na Hamuli.

6. Na wana wa Zera; Zabdi, na Ethani, na Hemani, na Kalkoli, na Darda; hao wote ni watano.

7. Na wana wa Karmi; Akani, yule mwenye kutaabisha Israeli, aliyekosa katika kitu kilichowekwa wakfu.

8. Na wana wa Ethani; Azaria.

9. Tena wana wa Hesroni aliozaliwa; Yerameeli, na Ramu, na Kalebu.

1 Nya. 2