1 Nya. 2:13-22 Swahili Union Version (SUV)

13. na Yese akamzaa Eliabu, mzaliwa wake wa kwanza, na wa pili Abinadabu, na wa tatu Shama;

14. na wa nne Nethaneli, na wa tano Radai;

15. na wa sita Ozemu, na wa saba Daudi;

16. na maumbu yao ni Seruya, na Abigaili. Na wana wa Seruya walikuwa, Abishai, na Yoabu, na Asaheli; hao watatu.

17. Na Abigaili akamzaa Amasa; na babaye Amasa ni Yetheri, Mwishmaeli.

18. Basi Kalebu, mwana wa Hesroni, akazaliwa wana na mkewe Azubu, na Yeriothi, na hawa ndio wanawe wa kiume; Yesheri, na Shobabu, na Ardoni.

19. Akafa Azuba, naye Kalebu akamtwaa Efrathi, aliyemzalia Huri.

20. Naye Huri akamzaa Uri; na Uri akamzaa Besaleli.

21. Na baadaye Hesroni akamwingilia binti wa Makiri, babaye Gileadi; ambaye alimtwaa alipokuwa mwenye miaka sitini; naye akamzalia Segubu.

22. Na Segubu akamzaa Yairi, aliyekuwa mwenye miji ishirini na mitatu katika nchi ya Gileadi.

1 Nya. 2