1 Nya. 2:12-20 Swahili Union Version (SUV)

12. na Boazi akamzaa Obedi; na Obedi akamzaa Yese;

13. na Yese akamzaa Eliabu, mzaliwa wake wa kwanza, na wa pili Abinadabu, na wa tatu Shama;

14. na wa nne Nethaneli, na wa tano Radai;

15. na wa sita Ozemu, na wa saba Daudi;

16. na maumbu yao ni Seruya, na Abigaili. Na wana wa Seruya walikuwa, Abishai, na Yoabu, na Asaheli; hao watatu.

17. Na Abigaili akamzaa Amasa; na babaye Amasa ni Yetheri, Mwishmaeli.

18. Basi Kalebu, mwana wa Hesroni, akazaliwa wana na mkewe Azubu, na Yeriothi, na hawa ndio wanawe wa kiume; Yesheri, na Shobabu, na Ardoni.

19. Akafa Azuba, naye Kalebu akamtwaa Efrathi, aliyemzalia Huri.

20. Naye Huri akamzaa Uri; na Uri akamzaa Besaleli.

1 Nya. 2