3. Tena Daudi akazidi kuoa wake huko Yerusalemu; akazidi Daudi kuzaa wana na binti.
4. Na haya ndiyo majina ya watoto aliozaliwa huko Yerusalemu; Shamua, na Shobabu, na Nathani, na Sulemani;
5. na Ibhari, na Elishua, na Elpeleti;
6. na Noga, na Nefegi, na Yafia;
7. na Elishama, na Eliada, na Elifeleti.