1 Nya. 14:13-17 Swahili Union Version (SUV)

13. Lakini hao Wafilisti wakateka nyara tena mara ya pili bondeni.

14. Na Daudi akamwuliza Mungu tena; naye Mungu akamwambia, Hutapanda kuwafuata; uwageukie mbali, ukawajie huko kuielekea miforsadi.

15. Kisha itakuwa utakapoisikia sauti ya kwenda katika vilele vya miforsadi, ndipo utakapokwenda nje vitani; kwa maana ndipo Mungu ametoka mbele yako, awapige jeshi la Wafilisti.

16. Daudi akafanya kama vile Mungu alivyomwamuru; wakawapiga jeshi la Wafilisti toka Geba mpaka Gezeri.

17. Sifa za Daudi zikafika nchi zote; naye BWANA akawaletea mataifa yote hofu yake.

1 Nya. 14