1 Nya. 12:6-15 Swahili Union Version (SUV)

6. Elkana, na Ishia, na Azaleli, na Yoezeri, na Yashobeamu, Wakora;

7. na Yoela, na Zebadia, wana wa Yerohamu, wa Gedori.

8. Na wa Wagadi wakajitenga kumfuata Daudi ngomeni huko nyikani, waume mashujaa, watu waliozoea vita, walioweza kutumia ngao na mkuki; ambao nyuso zao zilikuwa kama nyuso za simba, nao walikuwa wepesi kama kulungu juu ya milima;

9. Ezeri mkubwa wao, Obadia wa pili, Eliabu wa tatu;

10. Mishmana wa nne, Yeremia wa tano;

11. Atai wa sita, Elieli wa saba;

12. Yohana wa nane, Elzabadi wa kenda;

13. Yeremia wa kumi, Makbanai wa kumi na moja.

14. Hao wa wana wa Gadi walikuwa maakida wa jeshi, yeye aliyekuwa mdogo amelingana na mia, na yeye aliyekuwa mkuu, na elfu.

15. Hao ndio wale waliovuka Yordani katika mwezi wa kwanza, ulipofurika kingo zake zote; nao wakawakimbiza wote wa bondeni kuelekea mashariki na magharibi pia.

1 Nya. 12