1 Nya. 1:32-48 Swahili Union Version (SUV)

32. Na wana wa Ketura, suria yake Ibrahimu; yeye akamzaa Zimrani, na Yokshani, na Medani, na Midiani, na Ishbaki, na Shua. Na wana wa Yokshani; Sheba na Dedani.

33. Na wana wa Midiani; Efa, na Eferi, na Hanoki, na Abida, na Eldaa. Hao wote ndio wana wa Ketura.

34. Na Ibrahimu naye akamzaa Isaka. Wana wa Isaka; Esau, na Israeli.

35. Wana wa Esau; Elifazi, na Reueli, na Yeushi, na Yalamu, na Kora.

36. Wana wa Elifazi; Temani, na Omari, na Sefo, na Gatamu, na Kenazi, na, kwa Timna, Amaleki.

37. Wana wa Reueli; Nahathi, na Zera, na Shama, na Miza.

38. Na wana wa Seiri; Lotani, na Shobali, na Sibeoni, na Ana, na Dishoni, na Eseri, na Dishani.

39. Na wana wa Lotani; Hori, na Hemamu; na Timna ni umbu lake Lotani.

40. Wana wa Shobali; Alvani, na Manahathi, na Ebali, na Shefo, na Onamu. Na wana wa Sibeoni; Aya, na Ana.

41. Wana wa Ana; Dishoni. Na wana wa Dishoni; Hemdani, na Eshbani, na Ithrani, na Kerani.

42. Wana wa Eseri; Bilhani, na Zaawani, na Akani. Wana wa Dishani; Usi, na Arani.

43. Basi hawa ndio wafalme waliomiliki katika nchi ya Edomu, kabla hajamiliki mfalme awaye yote juu ya wana wa Israeli; Bela, mwana wa Beori; na jina la mji wake ni Dinhaba.

44. Bela akafa, naye Yobabu, mwana wa Zera, wa Bosra, akamiliki badala yake.

45. Yobabu akafa, naye Hushamu, wa nchi ya Watemani, akamiliki badala yake.

46. Hushamu akafa, naye Hadadi, mwana wa Bedadi, akamiliki badala yake, ambaye aliwapiga Midiani katika uwanja wa Moabu; na jina la mji wake ni Avithi.

47. Hadadi akafa, naye Samla, wa Masreka, akamiliki badala yake.

48. Samla akafa, naye Shauli, wa Rehobothi karibu na Mto, akamiliki badala yake.

1 Nya. 1