1 Nya. 1:17-32 Swahili Union Version (SUV)

17. Wana wa Shemu; Elamu, na Ashuru, na Arfaksadi, na Ludi, na Aramu, na Usi, na Huli, na Getheri, na Mashi.

18. Na Arfaksadi akamzaa Sala, na Sala akamzaa Eberi.

19. Na Eberi akazaliwa wana wawili wa kiume; jina la wa kwanza aliitwa Pelegi, maana katika siku zake nchi iligawanyika; na jina la nduguye aliitwa Yoktani.

20. Na Yoktani akamzaa Almodadi, na Shelefu, na Hasarmawethi, na Yera;

21. na Hadoramu, na Uzali, na Dikla;

22. na Obali, na Abimaeli, na Sheba;

23. na Ofiri, na Havila, na Yobabu. Hao wote ndio wana wa Yoktani.

24. Shemu, na Arfaksadi, na Sala;

25. na Eberi, na Pelegi, na Reu;

26. na Serugi, na Nahori, na Tera;

27. na Abramu, naye ndiye Ibrahimu.

28. Wana wa Ibrahimu; Isaka, na Ishmaeli.

29. Hivi ndivyo vizazi vyao; mzaliwa wa kwanza wa Ishmaeli, Nebayothi; kisha Kedari, na Abdeeli, na Mibsamu;

30. na Mishma, na Duma, na Masa, na Hadadi, na Tema;

31. na Yeturi, na, Nafishi, na Kedema. Hao ndio wana wa Ishmaeli.

32. Na wana wa Ketura, suria yake Ibrahimu; yeye akamzaa Zimrani, na Yokshani, na Medani, na Midiani, na Ishbaki, na Shua. Na wana wa Yokshani; Sheba na Dedani.

1 Nya. 1