1 Kor. 6:3-6 Swahili Union Version (SUV)

3. Hamjui ya kuwa mtawahukumu malaika, basi si zaidi sana mambo ya maisha haya?

4. Basi, mkiwa na mahali panapohukumiwa mambo ya maisha haya, mwawaweka kuwa waamuzi hao waliohesabiwa kuwa si kitu; katika kanisa?

5. Nasema hayo nipate kuwatahayarisha. Je! Ndivyo, kwamba kwenu hakuna hata mtu mmoja mwenye hekima, awezaye kukata maneno ya ndugu zake?

6. Bali mwashitakiana, ndugu kwa ndugu, tena mbele yao wasioamini.

1 Kor. 6