1 Kor. 16:6-10 Swahili Union Version (SUV)

6. Labda nitakaa kwenu; naam, labda wakati wote wa baridi, mpate kunisafirisha ko kote nitakakokwenda.

7. Maana sipendi kuonana nanyi sasa, katika kupita tu, kwa sababu nataraji kukaa kwenu muda kidogo, Bwana akinijalia.

8. Lakini nitakaa Efeso hata Pentekoste;

9. kwa maana nimefunguliwa mlango mkubwa wa kufaa sana, na wako wengi wanipingao.

10. Lakini, Timotheo akija, angalieni akae kwenu pasipo hofu; maana anaifanya kazi ya Bwana vile vile kama mimi mwenyewe;

1 Kor. 16