33. Msidanganyike; Mazungumzo mabaya huharibu tabia njema.
34. Tumieni akili kama ipasavyo, wala msitende dhambi; kwa maana wengine hawamjui Mungu. Ninanena hayo niwafedheheshe.
35. Lakini labda mtu atasema, Wafufuliwaje wafu? Nao huja kwa mwili gani?
36. Ewe mpumbavu! Uipandayo haihuiki, isipokufa;