31. Naam, ndugu, kwa huku kujisifu kwangu niliko nako juu yenu katika Kristo Yesu Bwana wetu, ninakufa kila siku.
32. Ikiwa, kwa jinsi ya kibinadamu, nalipigana na hayawani wakali kule Efeso, nina faida gani? Wasipofufuliwa wafu, na tule, na tunywe, maana kesho tutakufa.
33. Msidanganyike; Mazungumzo mabaya huharibu tabia njema.
34. Tumieni akili kama ipasavyo, wala msitende dhambi; kwa maana wengine hawamjui Mungu. Ninanena hayo niwafedheheshe.
35. Lakini labda mtu atasema, Wafufuliwaje wafu? Nao huja kwa mwili gani?
36. Ewe mpumbavu! Uipandayo haihuiki, isipokufa;
37. nayo uipandayo, huupandi mwili ule utakaokuwa, ila chembe tupu, ikiwa ni ya ngano au nyingineyo;
38. lakini Mungu huipa mwili kama apendavyo, na kila mbegu mwili wake.
39. Nyama yote si nyama moja; ila nyingine ni ya wanadamu, nyingine ya hayawani, nyingine ya ndege, nyingine ya samaki.