1 Kor. 15:3-7 Swahili Union Version (SUV)

3. Kwa maana naliwatolea ninyi hapo mwanzo yale niliyoyapokea mimi mwenyewe, ya kuwa Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu, kama yanenavyo maandiko;

4. na ya kuwa alizikwa; na ya kuwa alifufuka siku ya tatu, kama yanenavyo maandiko;

5. na ya kuwa alimtokea Kefa; tena na wale Thenashara;

6. baadaye aliwatokea ndugu zaidi ya mia tano pamoja; katika hao wengi wanaishi hata sasa, ila baadhi yao wamelala;

7. baadaye akamtokea Yakobo; tena na mitume wote;

1 Kor. 15