20. Lakini sasa Kristo amefufuka katika wafu, limbuko lao waliolala.
21. Maana kwa kuwa mauti ililetwa na mtu, kadhalika na kiyama ya wafu ililetwa na mtu.
22. Kwa kuwa kama katika Adamu wote wanakufa, kadhalika na katika Kristo wote watahuishwa.
23. Lakini kila mmoja mahali pake; limbuko ni Kristo; baadaye walio wake Kristo, atakapokuja.
24. Hapo ndipo mwisho, atakapompa Mungu Baba ufalme wake; atakapobatilisha utawala wote, na mamlaka yote, na nguvu.
25. Maana sharti amiliki yeye, hata awaweke maadui wake wote chini ya miguu yake.
26. Adui wa mwisho atakayebatilishwa ni mauti.