12. Basi, ikiwa Kristo anahubiriwa ya kwamba amefufuka katika wafu, mbona baadhi yenu husema kwamba hakuna kiyama ya wafu?
13. Lakini kama hakuna kiyama ya wafu, Kristo naye hakufufuka;
14. tena kama Kristo hakufufuka, basi, kuhubiri kwetu ni bure na imani yenu ni bure.
15. Naam, na sisi tumeonekana kuwa mashahidi wa uongo wa Mungu; kwa maana tulimshuhudia Mungu ya kuwa alimfufua Kristo, ambaye hakumfufua, ikiwa wafu hawafufuliwi.
16. Maana kama wafu hawafufuliwi, Kristo naye hakufufuka.
17. Na kama Kristo hakufufuka, imani yenu ni bure; mngalimo katika dhambi zenu.
18. Na hapo wao nao waliolala katika Kristo wamepotea.