1 Kor. 10:24-28 Swahili Union Version (SUV)

24. Mtu asitafute faida yake mwenyewe, bali ya mwenzake.

25. Kila kitu kiuzwacho sokoni kuleni, bila kuuliza-uliza, kwa ajili ya dhamiri;

26. maana, Dunia ni mali ya Bwana na vyote viijazavyo.

27. Na mtu asiyeamini akiwaalika, nanyi mnataka kwenda, kuleni kila kitu kiwekwacho mbele yenu bila kuuliza-uliza, kwa ajili ya dhamiri.

28. Lakini mtu akiwaambia, Kitu hiki kimetolewa kiwe sadaka, msile, kwa ajili yake yeye aliyeonyesha, na kwa ajili ya dhamiri.

1 Kor. 10