21. Hamwezi kushirikiana katika meza ya Bwana na katika meza ya mashetani.
22. Au twamtia Bwana wivu? Je! Tuna nguvu zaidi ya yeye?
23. Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vifaavyo. Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vijengavyo.
24. Mtu asitafute faida yake mwenyewe, bali ya mwenzake.
25. Kila kitu kiuzwacho sokoni kuleni, bila kuuliza-uliza, kwa ajili ya dhamiri;
26. maana, Dunia ni mali ya Bwana na vyote viijazavyo.
27. Na mtu asiyeamini akiwaalika, nanyi mnataka kwenda, kuleni kila kitu kiwekwacho mbele yenu bila kuuliza-uliza, kwa ajili ya dhamiri.
28. Lakini mtu akiwaambia, Kitu hiki kimetolewa kiwe sadaka, msile, kwa ajili yake yeye aliyeonyesha, na kwa ajili ya dhamiri.