1 Fal. 4:8-19 Swahili Union Version (SUV)

8. Na haya ndiyo majina yao. Mwana wa Huri, mlimani mwa Efraimu.

9. Mwana wa Dekari, kutoka Makasi, na Shaalbimu na Bethshemeshi na Elon-beth-hanani.

10. Mwana wa Hesedi, katika Arubothi; na Soko ilikuwa kwake na nchi yote ya Heferi.

11. Mwana wa Abinadabu katika Nafath-dori yote; ndiye aliyekuwa naye Tafathi binti Sulemani kuwa mke wake.

12. Baana mwana wa Ahiludi, katika Taanaki na Megido, na Beth-sheani yote, iliyo kando ya Sarethani, chini ya Yezreeli, tangu Beth-sheani mpaka Abel-mehola, hata kupita Yokmeamu.

13. Mwana wa Geberi katika Ramoth-gileadi; na kwake ilikuwa miji ya Yairi mwana wa Manase iliyomo Gileadi; na kwake ilikuwa wilaya ya Argobu, iliyomo Bashani, miji mikubwa sitini yenye kuta na makomeo ya shaba.

14. Ahinadabu mwana wa Ido, katika Mahanaimu.

15. Ahimaasi, katika Naftali; naye ndiye aliyemwoa Basemathi binti Sulemani.

16. Baana mwana wa Hushai, katika Asheri na Bealothi.

17. Yehoshafati mwana wa Parua, katika Isakari.

18. Shimei mwana wa Ela, katika Benyamini.

19. Geberi mwana wa Uri, katika nchi ya Gileadi, nchi ya Sihoni mfalme wa Waamori, na Ogu mfalme wa Bashani; naye alikuwa akida wa pekee katika nchi hiyo.

1 Fal. 4