4. Umenitetea kuhusu kisa changu cha haki;umeketi katika kiti chako cha enzi,ukatoa hukumu iliyo sawa.
5. Umeyakemea mataifa,umewaangamiza waovu;majina yao umeyafutilia mbali milele.
6. Maadui wameangamia milele;umeingolea mbali miji yao,kumbukumbu lao limetoweka.
7. Lakini Mwenyezi-Mungu anatawala milele;ameweka kiti chake cha enzi apate kuhukumu.
8. Anauhukumu ulimwengu kwa haki;anayaamua mataifa kwa unyofu.
9. Mwenyezi-Mungu ni ngome ya watu wanaoonewa;yeye ni ngome nyakati za taabu.
10. Wanaokujua wewe, ee Mungu hukutegemea,wewe Mwenyezi-Mungu huwatupi wakutafutao.
11. Mwimbieni sifa Mwenyezi-Mungu akaaye Siyoni.Yatangazieni mataifa mambo aliyotenda!