Zaburi 5:8-11 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Uniongoze, ee Mwenyezi-Mungu, katika uadilifu wako,maana maadui zangu ni wengi;uiweke njia yako wazi mbele yangu.

9. Vinywani mwao hamna ukweli;mioyoni mwao wamejaa maangamizi,wasemacho ni udanganyifu wa kifo,ndimi zao zimejaa hila.

10. Uwaadhibu kwa hatia yao ee Mungu;waanguke kwa njama zao wenyewe;wafukuze nje kwa sababu ya dhambi zao nyingi,kwa sababu wamekuasi wewe.

11. Lakini wafurahi wote wanaokimbilia usalama kwako,waimbe kwa shangwe daima.Uwalinde wanaolipenda jina lako,wapate kushangilia kwa sababu yako.

Zaburi 5