4. Heri mtu anayemtumainia Mwenyezi-Mungu;mtu asiyejiunga na watu wenye majivuno,watu waliopotoka kwa kuabudu miungu ya uongo.
5. Ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu, umetufanyia mengi ya ajabu,na mipango yako juu yetu haihesabiki;hakuna yeyote aliye kama wewe.Kama ningeweza kusimulia hayo yote,idadi yake ingenishinda.
6. Wewe hutaki tambiko wala sadaka,tambiko za kuteketeza wala za kuondoa dhambi;lakini umenipa masikio nikusikie.
7. Ndipo niliposema: “Niko tayari;ninayotakiwa kufanya yameandikwa katika kitabu cha sheria;
8. kutimiza matakwa yako, ee Mungu wangu ni furaha yangu,sheria yako naishika kwa moyo wangu wote!”
9. Nimesimulia habari njema za ukombozi,mbele ya kusanyiko kubwa la watu.Kama ujuavyo ee Mwenyezi-Mungu,mimi sikujizuia kuitangaza.
10. Sikuuficha moyoni mwangu ukombozi ulionijalia,nimetangaza daima kuwa wewe ni mwokozi mwaminifu;sikulificha kusanyiko kubwa la watufadhili zako na uaminifu wako.
11. Ee Mwenyezi-Mungu, usininyime huruma yako!Fadhili zako na uaminifu wako vinihifadhi daima.
12. Maafa yasiyohesabika yanizunguka,maovu yangu yanikaba hata siwezi kuona;ni mengi kuliko nywele kichwani mwangu,nami nimevunjika moyo.
13. Upende ee Mwenyezi-Mungu kuniokoa;ee Mwenyezi-Mungu, uje haraka kunisaidia.