Zaburi 40:2-7 Biblia Habari Njema (BHN)

2. Aliniondoa katika shimo la hatari,alinitoa katika matope ya dimbwi,akanisimamisha salama juu ya mwamba,na kuziimarisha hatua zangu.

3. Alinifundisha wimbo mpya,wimbo wa sifa kwa Mungu wetu.Wengi wataona na kuogopa,na kumtumainia Mwenyezi-Mungu.

4. Heri mtu anayemtumainia Mwenyezi-Mungu;mtu asiyejiunga na watu wenye majivuno,watu waliopotoka kwa kuabudu miungu ya uongo.

5. Ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu, umetufanyia mengi ya ajabu,na mipango yako juu yetu haihesabiki;hakuna yeyote aliye kama wewe.Kama ningeweza kusimulia hayo yote,idadi yake ingenishinda.

6. Wewe hutaki tambiko wala sadaka,tambiko za kuteketeza wala za kuondoa dhambi;lakini umenipa masikio nikusikie.

7. Ndipo niliposema: “Niko tayari;ninayotakiwa kufanya yameandikwa katika kitabu cha sheria;

Zaburi 40