Zaburi 39:1-3 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Nilisema: “Nitayachunga maisha yangu,nisije nikatenda dhambi kwa usemi wangu.Nitafunga mdomo wangu waovu wawapo karibu nami.”

2. Nilikuwa kama bubu, bila kusema kitu,nilinyamaza lakini sikupata nafuu.Mateso yangu yalizidi kuwa makali,

3. mahangaiko yangu yakaniunguza moyoni.Kadiri nilivyowaza ndivyo nilivyotaabika,kisha maneno haya yakanitoka:

Zaburi 39