Zaburi 38:9-19 Biblia Habari Njema (BHN)

9. Ee Bwana, wewe wajua tazamio langu lote;kwako hakikufichika kilio changu.

10. Moyo wanidunda, nguvu zimeniishia;hata macho yangu nayo yamekwisha fifia.

11. Rafiki na wenzangu wanaepa kuona mateso yangu,na jamaa zangu wanakaa mbali nami.

12. Wanaotaka kuniua wanatega mitego yao;wanaonitakia niumie wanatishia kuniangamiza.Mchana kutwa wanafanya mipango dhidi yangu.

13. Lakini mimi nimekuwa kama kiziwi, sisikii;nimekuwa kama bubu asiyeweza kusema kitu.

14. Naam, nimekuwa kama mtu asiyesikia,kama mtu asiye na chochote cha kujitetea.

15. Lakini ninakutumainia wewe, ee Mwenyezi-Mungu;wewe, ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu, ndiwe utakayenijibu.

16. Nakuomba tu maadui wasinisimange,wasione fahari juu ya kuanguka kwangu.

17. Karibu sana nitaanguka;nakabiliwa na maumivu ya daima.

18. Naungama uovu wangu;dhambi zangu zanisikitisha.

19. Maadui zangu hawajambo, wana nguvu;ni wengi mno hao wanaonichukia bure.

Zaburi 38