Zaburi 37:8-16 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Epuka hasira wala usiwe na ghadhabu;usihangaike maana hiyo huzidisha ubaya.

9. Watu watendao mabaya wataangamizwa,bali wanaomtumaini Mwenyezi-Mungu wataimiliki nchi.

10. Bado kitambo kidogo, naye mwovu atatoweka;utamtafuta pale alipokuwa, wala hutamwona.

11. Lakini wapole wataimiliki nchi,hao watafurahia wingi wa fanaka.

12. Mwovu hula njama dhidi ya mwadilifu,na kumsagia meno kwa chuki.

13. Lakini Mwenyezi-Mungu humcheka mwovu,kwani ajua mwisho wake u karibu.

14. Waovu huchomoa panga na kuvuta pinde zao,wapate kuwaua maskini na fukara;wawachinje watu waishio kwa unyofu.

15. Lakini panga zao zitawapenya wao wenyewe,na pinde zao zitavunjwavunjwa.

16. Afadhali mali kidogo ya mtu mwadilifukuliko utajiri wa watu waovu wengi.

Zaburi 37