20. Lakini waovu wataangamia,maadui za Mwenyezi-Mungu watanyauka kama maua nyikani;naam, watatoweka kama moshi.
21. Mtu mwovu hukopa bila kurudisha;lakini mwadilifu hutoa kwa ukarimu.
22. Waliobarikiwa na Mwenyezi-Mungu wataimiliki nchi,lakini waliolaaniwa naye watafutiliwa mbali.