Zaburi 37:15-20 Biblia Habari Njema (BHN)

15. Lakini panga zao zitawapenya wao wenyewe,na pinde zao zitavunjwavunjwa.

16. Afadhali mali kidogo ya mtu mwadilifukuliko utajiri wa watu waovu wengi.

17. Maana nguvu za waovu zitavunjwa,lakini Mwenyezi-Mungu huwategemeza waadilifu.

18. Mwenyezi-Mungu hutunza maisha ya watu waaminifu,na urithi wao utadumu milele.

19. Hawataaibika zikifika nyakati mbaya;siku za njaa watakuwa na chakula tele.

20. Lakini waovu wataangamia,maadui za Mwenyezi-Mungu watanyauka kama maua nyikani;naam, watatoweka kama moshi.

Zaburi 37