Zaburi 36:7-12 Biblia Habari Njema (BHN)

7. Jinsi gani zilivyo bora fadhili zako!Wanadamu hukimbilia kivulini mwa mabawa yako.

8. Wawashibisha kwa utajiri wa nyumba yako;wawanywesha kutoka mto wa wema wako.

9. Wewe ndiwe asili ya uhai;kwa mwanga wako twaona mwanga.

10. Uendelee kuwafadhili wale wanaokutambua;uzidi kuwa mwema kwa wanyofu wa moyo.

11. Usikubali wenye majivuno wanivamie,wala watu waovu wanikimbize.

12. Kumbe watendao maovu wameanguka;wameangushwa chini, hawawezi kuinuka.

Zaburi 36