7. Jinsi gani zilivyo bora fadhili zako!Wanadamu hukimbilia kivulini mwa mabawa yako.
8. Wawashibisha kwa utajiri wa nyumba yako;wawanywesha kutoka mto wa wema wako.
9. Wewe ndiwe asili ya uhai;kwa mwanga wako twaona mwanga.
10. Uendelee kuwafadhili wale wanaokutambua;uzidi kuwa mwema kwa wanyofu wa moyo.
11. Usikubali wenye majivuno wanivamie,wala watu waovu wanikimbize.
12. Kumbe watendao maovu wameanguka;wameangushwa chini, hawawezi kuinuka.