Zaburi 34:17-20 Biblia Habari Njema (BHN)

17. Waadilifu wakimlilia Mwenyezi-Mungu yeye huwasikia,na kuwaokoa katika taabu zao zote.

18. Mwenyezi-Mungu yu karibu na waliokufa moyo;huwaokoa wote waliokata tamaa kabisa.

19. Mateso ya mwadilifu ni mengi,lakini Mwenyezi-Mungu humwokoa kutoka yote.

20. Huvilinda viungo vya mwili wake wote,hakuna hata mfupa wake mmoja utakaovunjwa.

Zaburi 34