1. Nitamtukuza Mwenyezi-Mungu nyakati zote,sitaacha kamwe kuzitamka sifa zake.
2. Mimi nitaona fahari juu ya Mwenyezi-Mungu,wanyonge wasikie na kufurahi.
3. Mtukuzeni Mwenyezi-Mungu pamoja nami,sote pamoja tulisifu jina lake.
4. Nilimwomba Mwenyezi-Mungu naye akanijibu,na kuniondoa katika hofu zangu zote.
5. Mgeukieni Mungu mpate kufurahi;nanyi hamtaaibishwa kamwe.