Zaburi 33:17-20 Biblia Habari Njema (BHN)

17. Farasi wa vita hafai kitu kwa kupata ushindi;nguvu zake nyingi haziwezi kumwokoa mtu.

18. Mwenyezi-Mungu huwaangalia wale wamchao,watu ambao wanatumainia fadhili zake.

19. Yeye huwaokoa katika kifo,huwaweka hai wakati wa njaa.

20. Mioyo yetu yamtumainia Mwenyezi-Mungu.Yeye ni msaada wetu na ngao yetu.

Zaburi 33