Zaburi 31:19-24 Biblia Habari Njema (BHN)

19. Jinsi gani ulivyo mwingi wema wako,uliowawekea wale wanaokucha!Wanaokimbilia usalama kwakowawapa mema binadamu wote wakiona.

20. Wawaficha mahali salama hapo ulipo,mbali na mipango mibaya ya watu;wawaweka salama katika ulinzi wako,mbali na ubishi wa maadui zao.

21. Asifiwe Mwenyezi-Mungu,maana amenionesha fadhili zake kwa namna ya ajabu,nilipozingirwa kama mji unaoshambuliwa.

22. Nami niliogopa na kudhani kwamba ulikuwa umenitupa;kumbe, ulisikia kilio changu nilipokuita unisaidie.

23. Mpendeni Mwenyezi-Mungu, enyi watakatifu wake wote.Mwenyezi-Mungu huwalinda watu waaminifu;lakini huwaadhibu kabisa wenye kiburi wanavyostahili.

24. Muwe hodari na kupiga moyo konde,enyi nyote mnaomtumainia Mwenyezi-Mungu.

Zaburi 31