Zaburi 27:1-2 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Mwenyezi-Mungu ni mwanga wangu na wokovu wangu,ni nani nitakayemwogopa?Mwenyezi-Mungu ni ngome ya maisha yangu,sitamwogopa mtu yeyote.

2. Waovu wakinishambulia,na kutaka kuniangamiza,hao wapinzani wangu watajikwaa na kuanguka.

Zaburi 27