20. Iokoe nafsi yangu mbali na upanga,yaokoe maisha yangu makuchani mwa mbwa hao!
21. Uniokoe kinywani mwa simba;iokoe nafsi yangu dhaifu toka pembe za nyati hao.
22. Nitawasimulia ndugu zangu matendo yako;nitakusifu kati ya kusanyiko lao:
23. Enyi mnaomcha Mwenyezi-Mungu, msifuni!Mtukuzeni enyi wazawa wote wa Yakobo!Mcheni Mungu enyi wazawa wote wa Israeli!
24. Maana yeye hapuuzi au kudharau unyonge wa mnyonge;wala hajifichi mbali naye,ila humsikia anapomwomba msaada.
25. Kwa sababu yako ninakusifukatika kusanyiko kubwa la watu;nitatimiza ahadi zangu mbele yao wakuchao.