Zaburi 18:30-33 Biblia Habari Njema (BHN)

30. Huyu Mungu matendo yake hayana dosari!Ahadi ya Mwenyezi-Mungu ni ya kuaminika;yeye ni ngao kwa wote wanaomkimbilia usalama.

31. Nani aliye Mungu isipokuwa Mwenyezi-Mungu?Nani aliye mwamba wa usalama ila Mungu wetu?

32. Mungu ndiye anijaliaye nguvu kila upande;ndiye anayeifanya salama njia yangu.

33. Ameiimarisha miguu yangu kama ya paa,na kuniweka salama juu ya vilele.

Zaburi 18