30. Huyu Mungu matendo yake hayana dosari!Ahadi ya Mwenyezi-Mungu ni ya kuaminika;yeye ni ngao kwa wote wanaomkimbilia usalama.
31. Nani aliye Mungu isipokuwa Mwenyezi-Mungu?Nani aliye mwamba wa usalama ila Mungu wetu?
32. Mungu ndiye anijaliaye nguvu kila upande;ndiye anayeifanya salama njia yangu.
33. Ameiimarisha miguu yangu kama ya paa,na kuniweka salama juu ya vilele.