Zaburi 18:27-37 Biblia Habari Njema (BHN)

27. Wewe wawaokoa walio wanyenyekevu,lakini wenye majivuno huwaporomosha.

28. Wewe ee Mwenyezi-Mungu, waniangazia;walifukuza giza langu, ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu.

29. Kwa msaada wako nakishambulia kikosi;wewe wanipa nguvu ya kuruka ukuta.

30. Huyu Mungu matendo yake hayana dosari!Ahadi ya Mwenyezi-Mungu ni ya kuaminika;yeye ni ngao kwa wote wanaomkimbilia usalama.

31. Nani aliye Mungu isipokuwa Mwenyezi-Mungu?Nani aliye mwamba wa usalama ila Mungu wetu?

32. Mungu ndiye anijaliaye nguvu kila upande;ndiye anayeifanya salama njia yangu.

33. Ameiimarisha miguu yangu kama ya paa,na kuniweka salama juu ya vilele.

34. Hunifunza kupigana vita,mikono yangu iweze kuvuta upinde wa shaba.

35. Umenipa ngao yako ya kuniokoa;mkono wako wa kulia umenitegemeza;wema wako umenifanikisha.

36. Umenirahisishia njia yangu;wala miguu yangu haikuteleza.

37. Niliwafuatia adui zangu na kuwakamata;sikurudi nyuma mpaka nimewaangamiza.

Zaburi 18