17. Aliniokoa kutoka kwa maadui zangu wenye nguvu nyingi,aliniokoa kutoka kwa hao walionichukia,maana walikuwa na nguvu kunishinda.
18. Walinivamia nilipokuwa taabuni,lakini Mwenyezi-Mungu alikuwa kinga yangu.
19. Alinileta, akaniweka mahali pa usalama;alinisalimisha, kwani alipendezwa nami.
20. Mwenyezi-Mungu alinipa tuzo kadiri ya uadilifu wangu;alinituza kwa vile mikono yangu haina hatia.
21. Maana nimefuata njia za Mwenyezi-Mungu,wala sikujitenga na Mungu wangu kwa uovu.
22. Nimeshika maagizo yake yote,sikuacha kufuata masharti yake.
23. Mbele yake sikuwa na hatia;nimejikinga nisiwe na hatia.
24. Mwenyezi-Mungu amenituza kadiri ya uadilifu wangu;yeye ajua kwamba mikono yangu haina hatia.
25. Wewe ni mwaminifu kwa walio waaminifu;mwema kwa wale walio wema.
26. Wewe ni mkamilifu kwa walio wakamilifu;lakini mkatili kwa watu walio waovu.
27. Wewe wawaokoa walio wanyenyekevu,lakini wenye majivuno huwaporomosha.
28. Wewe ee Mwenyezi-Mungu, waniangazia;walifukuza giza langu, ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu.