10. Alipanda kiumbe chenye mabawa akaruka;akapaa kasi juu ya mabawa ya upepo.
11. Alijifunika giza pande zote,mawingu mazito yaliyojaa maji yalimzunguka.
12. Umeme ulimulika mbele yake;kukatokea mawinguni mvua ya mawe na makaa ya moto.
13. Mwenyezi-Mungu alinguruma kutoka mbinguni;Mungu Mkuu akatoa sauti yake,kukatokea mvua ya mawe na makaa ya moto.
14. Aliwapiga maadui mishale yake, akawatawanya,alirusha umeme, akawatimua.
15. Ulipowakemea maadui zako ee Mwenyezi-Mungu,ulipowatisha kwa ghadhabu yako,vilindi vya bahari vilifunuliwa,misingi ya dunia ikaonekana.