Yona 1:15-17 Biblia Habari Njema (BHN)

15. Basi, wakamchukua Yona, wakamtupa baharini, na papo hapo bahari ikatulia.

16. Mabaharia hao wakamwogopa sana Mwenyezi-Mungu, wakamtolea sadaka na kuweka nadhiri.

17. Kisha, Mwenyezi-Mungu akaamuru samaki mkubwa ammeze Yona, naye akawa tumboni mwa samaki huyo kwa muda wa siku tatu, usiku na mchana.

Yona 1