Yohane 5:8-10 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Yesu akamwambia, “Inuka, chukua mkeka wako utembee.”

9. Mara huyo mtu akapona, akachukua mkeka wake, akatembea. Jambo hili lilifanyika siku ya Sabato.

10. Kwa hiyo baadhi ya Wayahudi wakamwambia huyo mtu aliyeponywa, “Leo ni Sabato, si halali kubeba mkeka wako.”

Yohane 5