Yohane 21:9-11 Biblia Habari Njema (BHN)

9. Walipofika nchi kavu waliona moto wa makaa umewashwa na juu yake pamewekwa samaki na mkate.

10. Yesu akawaambia, “Leteni hapa baadhi ya samaki mliovua.”

11. Basi, Simoni Petro akapanda mashuani, akavuta hadi nchi kavu ule wavu uliokuwa umejaa samaki wakubwa 153. Na ingawa walikuwa wengi hivyo, wavu haukukatika.

Yohane 21