Yohane 20:1-3 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Alfajiri na mapema Jumapili, kukiwa bado na giza, Maria Magdalene alikwenda kaburini, akaliona lile jiwe limeondolewa mlangoni pa kaburi.

2. Basi, akaenda mbio hadi kwa Petro na yule mwanafunzi mwingine ambaye Yesu alimpenda, akawaambia, “Wamemwondoa Bwana kaburini, na wala hatujui walikomweka.”

3. Petro pamoja na yule mwanafunzi mwingine wakaenda kaburini.

Yohane 20