Yohane 19:32-35 Biblia Habari Njema (BHN)

32. Basi, askari walikwenda, wakaivunja miguu ya yule mtu wa kwanza na yule wa pili ambao walikuwa wamesulubiwa pamoja na Yesu.

33. Lakini walipomfikia Yesu, waliona kwamba alikwisha kufa, kwa hivyo hawakumvunja miguu.

34. Lakini askari mmoja alimtoboa ubavuni kwa mkuki, na mara ikatoka damu na maji. (

35. Naye aliyeona tukio hilo ameshuhudia ili nanyi mpate kuamini. Na hayo aliyosema ni ukweli, tena yeye anajua kwamba anasema ukweli).

Yohane 19