Yohane 17:3-7 Biblia Habari Njema (BHN)

3. Na uhai wa milele ndio huu: Kukujua wewe uliye peke yako Mungu wa kweli, na kumjua Yesu Kristo uliyemtuma.

4. Mimi nimekutukuza hapa duniani; nimeikamilisha ile kazi uliyonipa niifanye.

5. Sasa, Baba, nitukuze mbele yako kwa ule utukufu niliokuwa nao kabla ya kuumbwa ulimwengu.

6. “Nimekufanya ujulikane kwa watu wale ulionipa kutoka duniani. Walikuwa watu wako, nawe ukanipa wawe wangu; nao wamelishika neno lako.

7. Sasa wanajua kwamba kila ulichonipa kimetoka kwako.

Yohane 17