43. Walipendelea kusifiwa na watu kuliko kusifiwa na Mungu.
44. Kisha Yesu akasema kwa sauti kubwa, “Mtu anayeniamini, haniamini mimi tu, ila anamwamini pia yule aliyenituma.
45. Anayeniona mimi anamwona pia yule aliyenituma.
46. Mimi ni mwanga, nami nimekuja ulimwenguni ili wote wanaoniamini wasibaki gizani.