37. Ingawa Yesu alifanya miujiza hii yote mbele yao, wao hawakumwamini.
38. Hivyo maneno aliyosema nabii Isaya yakatimia:“Bwana, nani aliyeuamini ujumbe wetu?Na uwezo wa Bwana umedhihirishwa kwa nani?”
39. Hivyo hawakuweza kuamini, kwani Isaya alisema tena:
40. “Mungu ameyapofusha macho yao,amezipumbaza akili zao;wasione kwa macho yao,wasielewe kwa akili zao;wala wasinigeukie, asema Bwana,ili nipate kuwaponya.”