Yohane 12:37-40 Biblia Habari Njema (BHN)

37. Ingawa Yesu alifanya miujiza hii yote mbele yao, wao hawakumwamini.

38. Hivyo maneno aliyosema nabii Isaya yakatimia:“Bwana, nani aliyeuamini ujumbe wetu?Na uwezo wa Bwana umedhihirishwa kwa nani?”

39. Hivyo hawakuweza kuamini, kwani Isaya alisema tena:

40. “Mungu ameyapofusha macho yao,amezipumbaza akili zao;wasione kwa macho yao,wasielewe kwa akili zao;wala wasinigeukie, asema Bwana,ili nipate kuwaponya.”

Yohane 12