1. Hapo mwanzo, Neno alikuwako; naye alikuwa na Mungu, naye alikuwa Mungu.
2. Tangu mwanzo Neno alikuwa na Mungu.
3. Kwa njia yake vitu vyote viliumbwa; hakuna hata kiumbe kimoja kilichoumbwa pasipo yeye.
4. Yeye alikuwa chanzo cha uhai na uhai huo ulikuwa mwanga wa watu.