30. “Nitatoa ishara mbinguni na duniani;kutakuwa na damu, moto na minara ya moshi.
31. Jua litatiwa giza,na mwezi utakuwa mwekundu kama damu,kabla ya kufika siku ya Mwenyezi-Mungu,siku iliyo kuu na ya kutisha.
32. Hapo watu wote watakaoomba kwa jina la Mwenyezi-Mungu wataokolewa.Maana katika mlima Siyoni na Yerusalemu,watakuwako watu watakaosalimika,kama nilivyosema mimi Mwenyezi-Mungu.