Yoeli 1:9-11 Biblia Habari Njema (BHN)

9. Sadaka za nafaka na kinywaji zimetoweka nyumbani kwa Mwenyezi-Mungu.Makuhani, wahudumu wa Mwenyezi-Mungu, wanaomboleza.

10. Mashamba yamebaki matupu;nchi inaomboleza,maana nafaka imeharibiwa,divai imetoweka,mafuta yamekosekana.

11. Ombolezeni enyi wakulima;pigeni yowe enyi watunza mizabibu.Ngano na shayiri zimeharibika,mavuno yote shambani yameangamia.

Yoeli 1