9. Sadaka za nafaka na kinywaji zimetoweka nyumbani kwa Mwenyezi-Mungu.Makuhani, wahudumu wa Mwenyezi-Mungu, wanaomboleza.
10. Mashamba yamebaki matupu;nchi inaomboleza,maana nafaka imeharibiwa,divai imetoweka,mafuta yamekosekana.
11. Ombolezeni enyi wakulima;pigeni yowe enyi watunza mizabibu.Ngano na shayiri zimeharibika,mavuno yote shambani yameangamia.