Yobu 7:2-5 Biblia Habari Njema (BHN)

2. Yeye ni kama mtumwa atamaniye kivuli,kama mwajiriwa angojaye kwa hamu mshahara wake.

3. Basi nimepangiwa miezi na miezi ya ubatili,yangu ni majonzi usiku hata usiku.

4. Nilalapo nasema, ‘Nitaamka lini?’Kwani saa za usiku huwa ndefu sana;nagaagaa kitandani mpaka kuche!

5. Mwili wangu umejaa mabuu na uchafu;ngozi yangu imekauka na kutokwa na usaha wa jipu.

Yobu 7